Kocha wa Liverpool ameibuka na kusema kuumia kwa kiungo wa
Manchester City sio pigo hata kidogo kwani timu hiyo imesheheni wachezaji
lukuki wa kuziba pengo hilo. Kwa hivyo timu zingine za ligi kuu zisidhani
kutakua na wepesi watapo kutana na mabingwa hao.
“Ni mchezaji mzuri sana na nlikua nataka kumsajili pindi
yuko Chelsea ni nikiwa Dortmund ila Mourhino alikataa hivyo nawashangaa wanaona
ni afadhali kuumia kwake, mi siko hivyo kabisa sipendi kuona mchezaji anaemia na
hata awe timu pinzani na nnamuombea aweze kupona mapema na kurejea uwanjani, ”
aliongeza mchezaji huyo.
Klopp kagusia pia kikosi chake huku akiwaasa wachezaji wa
Liverpool kuahakutakua na mteremko kutokana na kikosi chake kuwa na wachezaji
wengi, “siwezi kufurahisha kila mtu kwa hivyo sitamvumilia mchezaji ambaye
ataleta mazingira hasi katika kikosi na nnawashauri wapiganie namba haswaaa
kwani hakuna nafasi kwa mzembe”, alionya Klopp.
Liverpool wanahusishwa kuleta ushindani mkubwa dhidi ya
Manchester City kuwania taji la ligi kuu kutokana na usajili wao wa kutisha
katika majira ya joto.
No comments:
Post a Comment