Ni kama uwanja wa dansi, Pep anenda anenda mbele hatua tano
na kisha kurud hatua nne, ankaa kisha ananyanyuka huku akitafuta maneno ya
kujazia kingereza chake hafifu anafoka tena, Sane akiwa kimya kasimama,
De-Bruyne yuko kimya mikono machoni, Silva kaegemea ukuta huku kaangalia chini.
Wachezaji na timu nzima ya ufundi ya Manchester City wakionekana
kuzoea hali hii kwani si mara ya kwanza kutokea, ilitokea wakati wa mapumziko
za kipindi cha kwanza cha fainali ya kombe la karabao dhibi ya Arsenal huku
Manchester city wakiwa wanongoza goli moja bila.
Pep anataka umakini, anataka ufanisi na yote anataka ushindi
kwa kila mechi hayo ni baadhi ya machache unayo weza kueleza juu ya mhispaniola
huyu.
Katika mapunziko ya mechi yao dhidi ya Manchester United
ambapo kila mchezaji alidhani mechi hiyo wameshinda na kunyakua kombe baada ya
wao kuwa mbele kwa mabao mwaili bila ilizua mjadala mkubwa baada ya mechi
kuisha, kwani Manchester United walirejesha mabao yote mawali na kuongeza la
tatu la ushindi.
Hali katitka vyumba vya kubadilishia vya Man City ilikua
tete huku Company na Delph wakionekana wenye sauti kubwa Yaya toure akiwa na mchango
pia katika vyumba hivyo.’si ni wa hovyo!....kipa wa hovyo, mabeki wa hovyo,viungo
wa kati wa hovyo na washabuliaji wa hovyo pia.’ Alisikika delph.
Wakati huo nahodha wa timu hiyo akijaribu kuwatuliza kwa
maneno ya busara “jamani sisi ni wachezaji wazuri, tangia msimu umeanza
tumecheza vizuri hadi hapa tulipo ila leo tumefungwa na sio kitu kizuri labda
inawezekana kwasababu ya uchovu” alinena nahodha huyo.
“Tumechoka? Hapana sisi ni wapuuzi…kipindi cha pili tuliacha
kukimbia, tuliacha kucheza hii haikubaliki” aling’aka Delph.
Baada ya kuzozana wao kwa wao Pep aliingilia kati na kusema ”mpira
sio maua, mpira sio kwenda likizo ila mpira ni mchezo wenye changamoto nyingi
cha msingi ni wachezaji kujitambua kama wa kimataifa na kusimamam kidete
kutoruhusu hali hii kutokea tena”.
Umoja, mshikamano na hari ya ushindi ndio vitu ambavyo Pep
anaweka kwa wachezaji wake na hivyo kuwafanya wajiskie vibaya sana washipo
shinda na pia kuongeza juhudi pia wanaposhinda ili washinde Zaidi.
Itaendelea……….
No comments:
Post a Comment