Kocha mpya wa Chelsea ameisifu timu yake baada ya ushindi wa
tatu bila majibu dhidi ya Huddersfield katika uwanja wa John Smith. Magolli ya Chelsea
yakiwa yamefungwa na Jiorghino kwa mkwaju wa penati, Kante na Pedro.
“ni kweli kipindi cha kwanza kilikua kigumu, tulishindwa
kucheza mpira nahii nadhani ni kwasababu wachezaji hawajazoea mfumo wa 5-3-1-1,
ila wakiuzoea tu basi itakua timu tofauti ” alisema sari.
Sarri amepanga kuifanya Chelsea iwe ya tofauti kwa kuwa na
mpira wa kasi na kuvutia kitu ambacho mara nyingi mliki wa klabu hiyo huwa
anatamani,”sitaki kuifanya chelsea iwe kaba Napoli ila nataka kuifanya iwe timu
bora kabisa na icheze mpira mzuri” aliongeza kocha huyo.
Muitaliano huyo alijiunga na Chelsea akitokea Napoli baada
ya kombe la dunia kuisha na hivyo kua na muda mfupi wa kuji andaa na ligi, ujio
wa kocha uyo ulifungua milango kwa kocha wa zamani wa klabu hiyo Antonio Conte.
Chelsea sasa yakaa kileleni kwa kuwa na uwiano mkubwa wa
magoli ya kufunga na kufungwa yaan ikiwa na magoli matatu bila kuruhusu nyavu
zao kuguswa.
No comments:
Post a Comment