Paul Pogba asema hawezi kuzungumza yaliyo moyoni mwake la
sivyo faini ita muhusu, kiungo huyo wa Manchester united amedokeza kuwa
anahitaji upendo tu awapo klabuni hapo ili kuonyesha makali yake ya kombe la
dunia.
Kiungo huyo mwenye miaka 25 alimaliza wiki kwa kishindo
baada ya kuingoza timu yake kuibuka na ushindi wa goli mbili moja dhidi ya Leicester
City akiwa kapteni, na kufuta uvumi wa kuhamia klabu ya Barcelona ilio kuwa iki
mmezea mate.
“Mimi ni yule yule wa kombe la dunia timu tu ndio tofauti,
inakua rahisi kucheza mpira pale unapokuwa na furaha na hasa unapoaminiwa na
kocha wako hivyo inaleta hamasa Zaidi vinginevyo ni karaha tupu”, alisema
kiungo huyo alipokua anagusia uhusiano wake na Mourhino ambao bad una mikwaruzo.
Na alisema maneno hayo kulinganisha kocha wake wa timu ya
taifa ya ufaransa dhidi ya kocha wake wa timu ya Manchester united, kiungo huyo
hakufurahia maneno ya Mourhino baada ya kombe la dunia.
No comments:
Post a Comment