Baada ya kuipatia timu yake bao la ushindi, Luke Shaw ambaye
msimu uliopita alikua na kiwango kibovu amesema kuwa anataka kufanya vizuri
katika ligi kuu ya msimu huu. Luke amesisitiza kuwa uwezo anao na nia anayo ya
kufanya vizuri licha ya watu ku-mbeza.
“Sitaki kuongea sana kwani bado mapema, ila nmekua nikafanya
juhudi kubwa ili kufikia malengo ninayo yataka na pia kuwaonyesha watu kuwa nia
ipo”,aliongeza mchezaji huyo.
Kocha wa mchezaji huyo hakuwa mchoyo wa fadhila baada ya
kumpongeza akisema “amefanya vizuri…Vizuri sana na sio tu kwa sababu alifunga,
la-hasha ila ni dadika 90 zote na pia alifanya kosa moja tu ambapo refa wa
pembeni angemsaidia kama angekua makina na kumpa faulo”.
Manchester united imeanza ligi kwa ushindi wa bao mbili kwa
moja dhidi ya Leicester city na kuifanya timu hiyo kukalia kiti cha msimamo wa
ligi, huku wapinzani wao wakitupwa mkiani.
Ligi hiyo itaendelea tena leo kwa mechi kadhaa kupigwa na
zingine zikifuata siku ya jumapili hivyo kukamilisha ufunguzi wa ligi.
No comments:
Post a Comment