Kocha wa Manchester United ameonyeshwa kutoridhika kwake na
katibu mkuu wa klabu hiyo ED Woodward kwa kushindwa kusajili wachezaji alio
wataka katika dirisha la usajili.
“nilikua na mipango mingi sana wakati dirisha la usajili
lilipofunguliwa na sikuwa nategemea kama mambo yangeishia hivi”, alisema
Mourhino.
“natamani sana ningekuwa na nafasi ya usemi katika kamati ya
usajili, nadhani kwakuwa ni kocha na sio maneja wa timu, mpira wa miguu
unabadilika na nafikiri mbeleni tutakuwa ni makocha tu sio mameneja ”.
“msimu huu utakua mgumu sana kwetu ila bado mapema ngoja
tuone hadi mwishoni wa novemba na mwanzoni mwa decemba, hapo ndio tutajua
tumesiamia wapi”.
“timu imefanya vizuri sana na Paul ni “mnyama” ameonesha
kiwango kikubwa huku akiwa na muda mfupi tu tangu arejee katika mazoezi, tulidhani
angehimili dakika 60 tu lakini hadi 80 alikuwa vizuri, Hatari sana! ” ,
aliongeza Mreno huyo alipoulizwa baada ya mechi.
No comments:
Post a Comment