Kiungo wa Manchester United Paul Pogba ameimbai klabu yake hiyo kuwa yuko tayari kui hama klabu hiyo na kutimkia Barcelona na hii imekuja tu baada ya mmiliki wake kusema kuwa wamuachie aondoke.
Taarifa za ndani zinasema kuwa Paul zasema kuwa kiungo huyo amekubaliana na miamba ya Hispania, Barcelona kitita cha paundi 3500000 kwa wiki. Paul amekua akiwataarifu wenzake kuwa ana mpango wa kutimka katika klabu hiyo.

Paul amekua na misimu miwili isiyo na tija kubwa kwa klabu hiyo ya mashetani wekundu na kumpelekea lawama zote kwa kocha wake, na hii kutokana na mfumo wa kocha huyo wa kulinda kuliko kushambulia.
Mourhino aliibuka na kukanusha vikali madai ya Paul na kusema kwamba kiungo huyu anapaswa kukaza buti na mfumo hauna mchango wowote katika kiwango chake bali yeye mwenyewe.
maneno hayo yalimtokea Mourhino puani baada ya kiungo huyo kufanya vizuri akiwa na kombe la dunia katika mfumo rafiki na uchezaji wake.
No comments:
Post a Comment