Mwakilishi wa kiungo wa Manchester United Paul Pogba amewasili nchini Uingereza kwa ajili ya mazungumzo na Klabu ya mteja wake juu ya mustakabali wa mteja wake huyo.
Huku vilabu kama Barcelona na Juventus zaendelea kumtolea macho kiungo huyo wa Ufaransa,Barceona ikiwa inasaka kiungo wa kucheza katikati kuziba pengo la mkongwe Andreas Iniesta alietimuka klabuni hapo.
Mourhino na Pogba wamekua na msimu ulijaa mikwaruzo ya hapa na pale kuhusu mbinu za kocha huyo ikiwemo na kiwango cha mfaransa kua na kiwango cha kupanda na kushuka na hivyo kujikuta akisugua benchi baadhi ya mechi.
Manchester ilambulia kichapo cha bao moja bila majibu dhidi ya mabingwa wa ujerumani na hivyo kuihitimisha “pre-season” kwa vichapo vya kutosha.
No comments:
Post a Comment