Mshambuliaji matata wa Manchster United arejea baada ya mapunziko yake ya kombe la dunia, mshambuliaji ameinekana katika gari yake binafsi akiwasili uwanja wa mazoezi wa Carington.
Lukaku hakujiunga na timu yake wakati wa maandalizi ya msimu mpya kutokana na kuwa na mapumziko baada ya kombe la dunia, hivyo hatarajiwi kuanza mechi dhidi ya Leicester city itakayo pigwa ijumaa ikiwa ni mechi ya kwanza ya ligi.
Ikumbukwe Manchester ilimaliza msimu wa maandalizi ya msimu mpya kwa kichapo cha bao moja bila kutoka kwa Bayern huku mreno huyo akisema kuwa “Afadhali imemalizika! Yalikua ni maandalizi marefu na magumu kwetu, nawapongeza wachezaji kwa kujituma ”.
Klabu hiyo ya jijini Manchester yaendelea kufanya maongezi ya kumnasa mlinzi wa kati wa Bayern huku dili la mlinzi Yerry Mina laonekana kugeuka dirisha.
No comments:
Post a Comment